Imani Ya Kibahá’í

Tovuti ya jumuiya ya Kibahá’í ya kiulimwengu

Vidokezo vya Jitihada ya Miaka Mia Moja

Mnamo 1921, wakati wa kufariki kwa ‘Abdu’l-Bahá, jumuiya ya ndogo ya Wabahá’í, ingawa ilikuwa na huzuni, ilitazamia siku za usoni kwa imani na ujasiri, ikizingatia maagizo ambayo yalikuwa yameachwa na Yeye, Kitovu cha Agano la Bahá’u’lláh. ‘Abdu’l-Bahá alikuwa ametoa mwongozo wa wazi wa jinsi jumuiya ya Wabahá’í ingekua, kuendelea na kuzidi kuwatumikia wanadamu. Tangu wakati huo, wafuasi wa Bahá’u’lláh wamekuwa wakijitahidi, kwa dhabihu isiyoweza kufikirika, kutekeleza mwongozo huo, kufikia pembe za mbali zaidi za dunia. Filamu hii inatoa dondoo za miaka mia moja ya juhudi na kujifunza, vilivyofanywa na jumuiya ya Wabahá'í inayoendelea kukua, na inaelezea safari ambayo imesababisha jitihada za sasa za jumuiya hii kuchangia kwenye kuibuka kwa ulimwengu unaozingatia kanuni ya umoja wa binadamu.

Before downloading please refer to the Terms of use