Bahá’u’lláh na Ahadi Yake
Asili ya Imani ya Kibahá’í na chanzo cha umoja wake wa kipekee
Tovuti ya jumuiya ya Kibahá’í ya kiulimwengu
Imani Ya Kibahá’í
Katika maelfu kwa maelfu ya maeneo kote ulimwenguni, mafundisho ya Imani ya Kibahá’í yanawavutia watu binafsi na jumuiya wanapojitahidi kuboresha maisha yao wenyewe na kuchangia kwenye uendelezaji wa ustaarabu. Itikadi za Kibahá’í hushughulikia mada muhimu sana kama vile umoja wa Mungu na dini, umoja wa binadamu na uhuru kutokana na chuki au mapenzi yasiyo na sababu, asili bora ya mwanadamu, ufunuo uendeleao wa ukweli wa kidini, ukuzaji wa sifa za kiroho, muungano wa ibada na huduma, usawa wa kimsingi wa jinsi, upatano kati ya dini na sayansi, umuhimu mkuu wa haki katika jitihada zote za kibinadamu, umuhimu wa elimu, na mienendo ya uhusiano ambao utawaunganisha pamoja watu binafsi, jumuiya, na asasi, kadri jamii ya binadamu isongavyo mbele kuelekea ukomavu wake wa pamoja.
Yeye Ambaye ni Bwana wenu, Mwenye-Rehema Zote, huthamini moyoni Mwake shauku ya kuona mbari nzima ya binadamu kama roho moja na mwili mmoja.
Asili ya Imani ya Kibahá’í na chanzo cha umoja wake wa kipekee
Roho ya milele, kusudi la maisha, na maendeleo ya sifa za kiroho
Mungu, ufunuo, binadamu, ulimwengu wa asili, na uendelezaji wa ustaarabu
Maendeleo ya uhusiano baina ya watu binafsi, jumuiya, na taasisi ambao unaakisi kanuni ya umoja wa binadamu
Ili kupata utambuzi kamili wa itikadi za Kibahá’í huenda utataka kutembelea Maktaba ya Kibahá’í ya Marejeo ambako unaweza kusoma Maandiko ya Báb, Bahá’u’lláh, na ‘Abdu’l-Bahá pamoja na juzuu zilizoandikwa na Shoghi Effendi na teuzi la matamko na mawasiliano ya Nyumba ya Haki ya Ulimwengu.
Tembelea Maktaba
— Bahá’u’lláh —