Kile Wabahá’í Wanachoamini
Mtu Binafsi na Jamii
Utangulizi
- Kile Wabahá’í Wanachoamini
- Maelezo ya jumla
- Bahá’u’lláh na Ahadi Yake
- Maisha ya roho
- Mungu na Muumbo Wake
- Mahusiano ya Kimsingi
- Amani ya Ulimwengu
- Kile Wabahá’í wanachofanya
Leo tunaishi katika kipindi cha kipekee katika historia. Kadri wanadamu wanavyojitokeza kutoka utoto na kukaribia ukomavu wake wa pamoja, hitaji la uelewa mpya wa mahusiano kati ya mtu binafsi, jumuiya, na asasi za jamii unazidi kuwa wa umuhimu zaidi.
Utegemezi mmoja kwa mwingine wa wahusika hawa watatu katika uendelezaji mbele wa ustaarabu lazima utambuliwe na mifano ya awali ya ugomvi, ambamo kwa mfano, asasi zinashurutisha utii ilhali watu binafsi hupiga kelele wakidai uhuru, inahitaji kubadilishwa na dhana za kina zaidi za majukumu yanayokamilishana yanayopaswa kutekelezwa na kila mmoja katika kujenga ulimwengu bora zaidi.
Kukiri kwamba mtu binafsi, jumuiya, na asasi za jamii ni wahusika wakuu wa ujengaji ustaarabu, na kutenda ipasavyo, hufungua uwezekano kubwa kwa furaha ya binadamu na huruhusu uundaji wa mazingira ambamo uwezo wa kweli wa roho ya binadamu unaweza kuachiwa huru.
Watu wote wameumbwa kupeleka mbele ustaarabu uendeleao daima.







