“Sema: Ulimwengu wa Kiasili katika kiini chake ni mfano halisi wa Jina Langu, Mfanyaji, Muumba.” – Bahá’u’lláh

Ulimwengu wa Kiasili

Ulimwengu wa Asili,Bahá’u’lláh huandika, “ni Majaliwa ya Mungu na ni kujieleza kwake katika na kupitia ulimwengu mtegemezi.” Ni mfano halisi wa jina la Mungu, “Muumba.

‘Abdu’l-Bahá alitoa wazo kwamba binadamu watakuwa “daima wanachukua vitu vipya na vya ajabu kutoka maabara ya ulimwengu wa asili.” Kadri tunavyojifunza namna nzuri kabisa ya kutumia malighafi za ulimwengu ili kuendeleza mbele ustaarabu, yatubidi kuzingatia mitazamo yetu juu ya chanzo cha riziki yetu na utajiri.

Kuona uakisi wa sifa za Mungu katika ulimwengu wa asili na kuzielewa kama kielelezo cha mapenzi Yake huchochea ndani yetu heshima ya kina kwa ulimwengu wa asili. Lazima hii isiangaliwe kama mwito kuuabudu ulimwengu wa asili. Binadamu wana uwezo kujiweka huru kutoka ulimwengu wa asili; “kwa muda wote ambao mwanadamu ni mateka wa ulimwengu wa asili yeye ni mnyama mkali, kwa kuwa mapambano kwa ajili ya kuishi ni moja kati ya mahitaji ya dharura ya ulimwengu wa asili.” Hata hivyo, ulimwengu wa asili ni amana takatifu ambayo wajumbe wote wa familia moja ya binadamu—kama waangalizi wa maliasili nyingi mno za sayari—wanawajibikia.


“Tunahitaji mabadiliko ya moyo, kuumbwa upya kwa mawazo yetu yote na mwelekeo mpya wa shughuli zetu. Maisha ya ndani ya mtu pamoja na mazingira yake ya nje lazima yaundwe upya ikiwa ukombozi wa binadamu unatakiwa kufikiwa.”

— Kutoka barua iliyoandikwa kwa niaba ya Shoghi Effendi

{{ note }}: